Wakolosai 4:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua ya kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2
Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru.
3
Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.
4
Ombeni ili nipate kuitangaza Injili kwa udhahiri kama ipasavyo kunena.
Settings