Skip to content
Wakolosai 3:5-10

Wakolosai 3:5-10

5
Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
6
Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
7
Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
8
Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
9
Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
10
nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options