Skip to content
1 Wathesalonike 5:4-8

1 Wathesalonike 5:4-8

4
Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
5
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
6
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
7
Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
8
Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options