1 Wathesalonike 5:4-8
4
Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
5
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
6
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
7
Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
8
Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Settings