1 Samweli 8:1-5
1
Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
2
Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
3
Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
4
Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
5
Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
Settings