Skip to content
1 Wakorintho 15:50-57

1 Wakorintho 15:50-57

50
Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
51
Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
52
ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
53
Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
54
Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
55
“Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?”
56
Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
57
Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options