Skip to content
1 Nyakati 16:23-33

1 Nyakati 16:23-33

23
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options