Rukia maudhui

Zaburi112

Heri Kumcha BWANA

1
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.

Thawabu za Mwenye Haki na Wazao Wake

2
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.

Tabia ya Mtu Mwenye Huruma

4
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.

Usalama na Kumbukumbu Isiyokufa

6
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.

Hatima ya Mwisho ya Waovu

10
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options