- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi103
Listen to this chapter
0:00
0:00
Ee Nafsi Yangu, Ubariki Bwana
1
Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.
2
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,
3
akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,
4
aukomboa uhai wako na kaburi, akuvika taji ya upendo na huruma,
5
atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
Haki ya Bwana na Rehema Zake Nyingi
6
Bwana hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
7
Alijulisha Mose njia zake, na wana wa Israeli matendo yake.
Fadhili za Bwana Zisizokoma
8
Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo.
9
Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele,
10
yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.
11
Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha;
12
kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi.
13
Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;
14
kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.
15
Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la shambani;
16
upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena.
17
Lakini kutoka milele hata milele upendo wa Bwana uko kwa wale wamchao, nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao:
18
kwa wale walishikao agano lake na kukumbuka kuyatii mausia yake.
Enzi Kuu ya Mungu Juu ya Vyote na Sifa za Ulimwengu
19
Bwana ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, ufalme wake unatawala juu ya vyote.
20
Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake, ninyi mnaotii neno lake.
21
Mhimidini Bwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake.
22
Mhimidini Bwana, kazi zake zote kila mahali katika milki yake. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note