- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mithali7
Listen to this chapter
0:00
0:00
Shikamana na Hekima
1
Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
2
Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3
Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
4
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
5
watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
Kumchunguza Kijana Mpumbavu
6
Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
7
Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
8
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
9
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
10
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
11
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
12
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
13
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
14
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
15
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
16
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
17
Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
18
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
19
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
20
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
21
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
22
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
23
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
Onyo la Mwisho Dhidi ya Uasherati
24
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
25
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
26
Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
27
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note