Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu The Euphrates

7 mistari · 14 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:

  2. “Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”

  3. Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.

  4. Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”

  5. Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.

  6. Ndipo neno la Bwana likanijia:

  7. “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.