Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Hoof

12 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.

  2. “ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.

  3. Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  4. Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  5. Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.

  6. Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.

  7. Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.

  8. Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,

  9. kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.

  10. Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.

  11. Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.

  12. Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.