Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Godly Fear

7 mistari · 50 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.

  2. Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”

  3. Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.

  4. Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.

  5. na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,

  6. na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

  7. ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.