Mistari ya Biblia kuhusu Goat: Designated as one of the clean animals to be eaten
Mistari kuhusu Designated as one of the clean animals to be eaten
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
“ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.