Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Gideon: Angel attests the call to, by miracle

4 mistari · 14 vipengele

Mistari kuhusu Angel attests the call to, by miracle

  1. Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.

  2. Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”

  3. Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”

  4. Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.