Skip to content
Zekaria 11:2

Zekaria 11:2

Inaonyesha mstari 2 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Fungua milango yako, ee Lebanoni, ili moto uteketeze mierezi yako!
2
Piga yowe, ee mti wa msunobari, kwa kuwa mwerezi umeanguka; miti ya fahari imeharibiwa! Piga yowe, enyi mialoni ya Bashani, msitu mnene umefyekwa!
3
Sikiliza yowe la wachungaji; malisho yao manono yameangamizwa! Sikia ngurumo za simba; kichaka kilichostawi sana cha Yordani kimeharibiwa!
4
Hili ndilo asemalo Bwana Mungu wangu: “Lilishe kundi lililokusudiwa kuchinjwa.
5
Wanunuzi wake huwachinja na kuondoka pasipo kuadhibiwa. Wale wanaowauza husema, ‘Bwana asifiwe, mimi ni tajiri!’ Wachungaji wao wenyewe hawawahurumii.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options