Rukia maudhui
Zaburi 84:8-12

Sala ya Kibali na Kumtumaini Mungu

Zaburi 84:8-12
8
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
9
Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
10
Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
11
Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
12
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options