Zaburi 81:3
Inaonyesha mstari 3 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
Settings