Zaburi 80:8-13
8
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Settings