Skip to content
Zaburi 78:60-67

Zaburi 78:60-67

60
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options