Skip to content
Zaburi 78:67-72

Zaburi 78:67-72

67
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options