Skip to content
Zaburi 78:56-59

Zaburi 78:56-59

56
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options