Zaburi 78:60-64
60
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Settings