Zaburi 78:56-64
56
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Settings