Skip to content
Zaburi 78:17-22

Zaburi 78:17-22

17
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options