Skip to content
Zaburi 73:6-11

Zaburi 73:6-11

6
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options