Zaburi 73:4-12
4
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Settings