Zaburi 73:3-9
3
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Settings