Zaburi 73:23-28
23
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Settings