Zaburi 73:21-26
21
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Settings