Rukia maudhui
Zaburi 69:22-29

Sala ya Hukumu ya Mungu

Zaburi 69:22-29
22
Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego, nayo iwe upatilizo na tanzi.
23
Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.
24
Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.
25
Mahali pao na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
26
Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi, na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
27
Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.
28
Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
29
Mimi niko katika maumivu na dhiki; Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options