Zaburi 65:1-4
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2
Ewe usikiaye maombi, kwako wewe watu wote watakuja.
3
Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi, wewe ulisamehe makosa yetu.
4
Heri wale uliowachagua na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako! Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako, mema ya Hekalu lako takatifu.
Settings