Zaburi 60:9-12
9
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
10
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
11
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
12
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Settings