Zaburi 57:7-11
7
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Settings