Zaburi 58:1-5
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Enyi watawala, je, kweli mwanena kwa haki? Je, mnahukumu kwa unyofu miongoni mwa watu?
2
La, mioyoni mwenu mnatunga udhalimu, na mikono yenu hupima jeuri duniani.
3
Waovu ni wapotovu tangu kuzaliwa kwao, toka tumboni mwa mama zao ni wakaidi na husema uongo.
4
Sumu yao ni kama sumu ya nyoka, kama ile ya fira ambaye ameziba masikio yake,
5
ambaye hatasikia sauti ya kutumbuiza ya mwaguzi, hata kama mganga angecheza kwa ustadi kiasi gani.
Settings