Zaburi 56:8-13
8
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Settings