Skip to content
Zaburi 50:18-20

Zaburi 50:18-20

18
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.

See also

Where else Scripture says this.

  • Mathayo 10:21

    “Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.
    from verse 20
  • Zaburi 10:7

    Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.
    from verse 19
  • 1 Timotheo 5:22

    Usiwe na haraka kumwekea mtu mikono wala usishiriki dhambi za watu wengine. Jilinde nafsi yako uwe safi.
    from verse 18
  • Warumi 1:32

    Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
    from verse 18
  • Waebrania 13:4

    Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
    from verse 18
  • Yeremia 9:5

    Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
    from verse 19
  • Zaburi 52:2

    Ulimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi. Ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila.
    from verse 19
  • Zaburi 52:4

    Unapenda kila neno lenye kudhuru, ewe ulimi wenye hila!
    from verse 19
  • Zaburi 55:21

    Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
    from verse 19
  • Ufunuo 21:8

    Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”
    from verse 19
  • Walawi 19:16

    “ ‘Usieneze uchochezi miongoni mwa watu wako. “ ‘Usifanye kitu chochote kile kinachohatarisha maisha ya jirani yako. Mimi ndimi Bwana.
    from verse 20
  • Mithali 10:18

    Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
    from verse 20
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options