Zaburi 50:17-20
17
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.