Zaburi 47:5-8
5
Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti za tarumbeta.
6
Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa, mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
7
Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote, mwimbieni zaburi za sifa.
8
Mungu anatawala juu ya mataifa, Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu.
Settings