Zaburi 47:1-4
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Pigeni makofi, enyi mataifa yote, mpigieni Mungu kelele za shangwe!
2
Jinsi gani alivyo wa kutisha, Bwana Aliye Juu Sana, Mfalme mkuu juu ya dunia yote!
3
Ametiisha mataifa chini yetu watu wengi chini ya miguu yetu.
4
Alituchagulia urithi wetu, fahari ya Yakobo, aliyempenda.
Settings