Zaburi 35:4-8
4
Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
5
Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
6
Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
7
Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
8
maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
Settings