Skip to content
Zaburi 35:4-12

Zaburi 35:4-12

4
Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
5
Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
6
Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
7
Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
8
maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
9
Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana na kuufurahia wokovu wake.
10
Nitapaza sauti yangu nikisema, “Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana? Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao, maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”
11
Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
12
Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options