Zaburi 35:16-18
16
Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
17
Ee Bwana, utatazama mpaka lini? Niokoe maisha yangu na maangamizi yao, uhai wangu wa thamani kutokana na simba hawa.
18
Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa, nitakusifu katikati ya watu wengi.