Rukia maudhui
Zaburi 34:15-20

Zaburi 34:15-20

15
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options