Zaburi 28:7-9
7
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.