Skip to content
Zaburi 17:10-12

Kiburi cha Maadui

Zaburi 17:10-12

Kiburi cha Maadui

10
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.

Jifunze kifungu hiki

Ufafanuzi wa kifungu hiki, si mstari mmoja.

Maandiko mengine yanaposema hivi.

  • 1 Samweli 2:3

    “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
    kutoka mstari wa 10
  • Zaburi 31:18

    Midomo yao isemayo uongo na inyamazishwe, kwa maana kwa kiburi na dharau wao husema kwa majivuno dhidi ya wenye haki.
    kutoka mstari wa 10
  • Zaburi 123:4

    Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi, dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.
    kutoka mstari wa 10
  • Mathayo 13:15

    Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
    kutoka mstari wa 10
  • Ufunuo 13:5

    Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
    kutoka mstari wa 10
  • Ufunuo 13:6

    Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
    kutoka mstari wa 10
  • Mithali 6:13

    ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
    kutoka mstari wa 11
  • Mithali 6:14

    ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
    kutoka mstari wa 11
  • Zaburi 37:14

    Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde, ili wawaangushe maskini na wahitaji, kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
    kutoka mstari wa 11
  • Zaburi 7:2

    la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
    kutoka mstari wa 12
  • 2 Petro 2:18

    Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
    kutoka mstari wa 10
  • Matendo 28:27

    Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
    kutoka mstari wa 10
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options