Zaburi 149:1-5
1
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Settings