Zaburi 149:6-9
6
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Settings