Skip to content
Zaburi 140:6-12

Zaburi 140:6-12

6
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options