Skip to content
Zaburi 13:1-4

Zaburi 13:1-4

1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako mpaka lini?
2
Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini?
3
Nitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4
Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options