Zaburi 119:161-168
161
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
162
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
163
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
164
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
165
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
166
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
167
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
168
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
Settings